Matthew 6:19-21

Akiba Ya Mbinguni

(Luka 12:33-34)

19 a “Msijiwekee hazina duniani, mahali ambapo nondo na kutu huharibu, nao wevi huvunja na kuiba. 20 bLakini jiwekeeni hazina mbinguni, mahali ambapo nondo na kutu haviharibu, wala wevi hawavunji na kuiba. 21 cKwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo pia moyo wako utakapokuwa.

Copyright information for SwhNEN